Friday, October 26, 2012

Mawakili wajitoa kumtetea Sheikh Farid, anyolewa ndevu

Sheik Farid Hadi Ahmed (kushoto juu) baada hajanyolewa ndevu na chini kabla ya kunyolewa ndevu

VIONGOZI wanane wa Jumuiya za Uamsho na Mihadhara ya Kiislamu Zanzibar (JUMIKI), akiwamo Sheikh Farid Hadi Ahmed jana walifikishwa mahakamani kwa mara ya pili, huku wakiwa wamenyolewa ndevu zao.
Sheikh Farid na viongozi wenzake walifikishwa mahakamani chini ya ulinzi mkali wa polisi na kufunguliwa mashtaka mawili.
Wakati wanafikishwa mahakamani kwa mara ya kwanza Oktoba 22 mwaka huu  washtakiwa wote walikuwa na ndevu nyingi videvuni mwao, lakini jana walikuwa wamenyolewa na kuwafanya wawe na mwonekano tofauti jambo ambalo lililozua gumzo kubwa miongoni mwa watu waliofika kusikiliza kesi hiyo.
Awali, viongozi hao walitarajiwa kufikishwa kwenye Mahakama ya Wilaya ya Mwanakwereke, badala yake walipelekwa Mahakama Kuu, Vuga mjini hapa na kufunguliwa mashtaka mapya.

Akiwasomea mashtaka watuhumiwa hao mbele ya Mrajisi wa Mahakama Kuu Zanzibar, George Kazi, Wakili wa Serikali, Raya Msellem alisema vitendo walivyofanya vinahatarisha amani Zanzibar, likiwamo tukio la Sheikh Farid Hadi Ahmed kutoweka hivi karibuni ambalo lilisababisha kuibuka ghasia kubwa visiwani humo.

Wengine waliofikishwa jana mahakamani ni masheikh Msellem Ali Msellem, Mussa Juma Issa, Azzan Khalid Hamdan, Suleiman Juma Suleiman, Khamis Ali Suleiman, Hassan Bakar Suleiman na Ghalib Ahmada Omar.

Wakili huyo alidai kuwa kuanzia Oktoba 17 hadi Oktoba 18, mwaka huu katika barabara kadhaa za Mkoa wa Mjini Magharibi washtakiwa hao walichochea wafuasi wao kuharibu barabara, kuvunja nyumba, kuharibu vyombo vya moto na kusababisha hasara ya Sh500 milioni.

Vilevile, Msellem alidai kuwa Mei 26 hadi Oktoba 19, mwaka huu katika maandamano yaliyofanyika Lumumba, Msumbiji, Fuoni Meli sita na Mbuyuni Unguja watuhumiwa wanadaiwa kuwashawishi watu wengine ambao hawapo kortini kufanya ghasia na kuhatarisha amani.
Baada ya mashtaka hayo, watuhumiwa hao walirudishwa tena Mahakama ya Mwanakwereke kuendelea na kesi yao ya awali. Hata hivyo, kesi hiyo haikuweza kusikilizwa kwa kuwa hakimu anayeisikiliza  hakuwapo mahakamani.

Washtakiwa hao wamerudishwa rumande hadi Novemba 7 kesi yao ya Mwanakwerekwe itakaposikilizwa na Novemba 8 wanatarajiwa kupanda tena kizimbani katika Mahakama Kuu kuendelea kusikiliza kesi yao.

Hata hivyo, watuhumiwa hao walifikishwa mahakamani bila ya kuwa na mawakili wao, Salim Tawfik na Abdallah Juma ambao wamejitoa katika kesi hiyo kwa madai ya kuwa wateja wao wanadhalilishwa.

Mawakili wajitoa
Wakizungumza na waandishi wa habari nje ya Mahakama Kuu Vuga, mawakili hao walisema kitendo cha Serikali kuwashikilia wateja wao na kushindwa kuwaleta mahakamani ni dalili tosha ya kuonyesha haki haiwezi kutendeka, kwani ni kitendo kinachokwenda kinyume na sheria za kimataifa na sheria za nchi kwamba dhamana ni haki ya kila raia.
“Inaonyesha hapa haki haiwezi kutendeka, dalili zimeanza kuonyesha mapema kwa sababu kwanza wamezuiliwa kupewa dhamana wakati pande zote mbili hazikuwa na pingamizi la kutoa dhamana, lakini mahakama ndiyo inakataa kutoa dhamana,”alisema Salim Tawfik.

Tawfik alisema jambo lingine la kushangaza ni kwamba washtakiwa walitakiwa kufikishwa Mahakama ya Mwanakwerekwe, lakini baadaye wakaambiwa wateja  wao wamepelekwa Mahakama Kuu ya Vuga na kwamba walipofika huko hawakuwakuta maofisa wa mahakama.

“ Tunajitoa katika hii kesi kwa leo (jana) ili kufikisha ujumbe kwa Serikali kwamba hawawatendei haki wateja wetu,” alisema.

Jumatatu iliyopita watu saba bila kuwamo Ghalib Ahmada Omar walifikishwa katika Mahakama ya Mwanakwerekwe kwa madai ya kufanya uchochezi katika mhadhara uliofanyika Agosti 17 mwaka huu.

2 comments:

oakleyses said...

chanel handbags, burberry outlet online, christian louboutin outlet, nike air max, oakley vault, tiffany and co jewelry, michael kors outlet online, michael kors handbags, burberry outlet online, ray ban sunglasses, michael kors outlet store, prada handbags, oakley sunglasses, kate spade outlet, christian louboutin shoes, michael kors outlet, longchamp handbags, christian louboutin, coach outlet store online, true religion outlet, louis vuitton outlet, longchamp outlet online, nike free, true religion, polo ralph lauren outlet, gucci handbags, louis vuitton handbags, coach outlet, louis vuitton outlet, prada outlet, nike air max, jordan shoes, nike outlet, polo ralph lauren, louis vuitton, longchamp outlet, red bottom shoes, tory burch outlet online, kate spade outlet online, michael kors outlet online, coach purses, ray ban outlet, michael kors outlet online, coach outlet, tiffany jewelry, cheap oakley sunglasses, louis vuitton outlet online

oakleyses said...

ferragamo shoes, soccer shoes, nike roshe, nfl jerseys, vans outlet, jimmy choo shoes, beats headphones, reebok shoes, valentino shoes, lululemon outlet, birkin bag, p90x workout, ugg outlet, asics shoes, mac cosmetics, longchamp, hollister, mcm handbags, ugg, babyliss, marc jacobs outlet, north face jackets, insanity workout, celine handbags, soccer jerseys, uggs on sale, canada goose outlet, wedding dresses, uggs outlet, replica watches, uggs outlet, canada goose, nike huarache, north face jackets, ugg boots clearance, mont blanc pens, instyler ionic styler, herve leger, nike trainers, canada goose outlet, canada goose outlet, giuseppe zanotti, new balance outlet, bottega veneta, ghd, ugg boots, chi flat iron, abercrombie and fitch, ugg soldes