Sunday, November 11, 2012

CCM Moto:Mpango wa Kumvua Kikwete Uenyekiti CCM Wasukwa

Mwenyekiti wa CCM Jakaya Kikwete

Moto ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) unazidi kuwaka, wakati wanaCCM wanakutana mjini Dodoma kwa siku tatu katika mkutano wake mkuu, ambao utachagua viongozi wa kitaifa watakaokiongoza chama hicho pamoja na wajumbe wa Nec 10 kutoka Tanzania Bara na wengine kumi kutoka Zanzibar.

Tayari kumekuwa na taarifa za mpango uliosukwa wa kutaka kudodosha Mwenyekiti wa CCM Jakaya Kikwete kwenye uchaguzi huo kwa lengo la kumpunguzia madaraka.

Kikwete alipowasili jana tayari kwa kuongoza Mkutano Mkuu 

Kumekuwa na vipeperushi ambavyo vimesambazwa huko Dodoma vikitaka wajumbe wa Mkutano Mkuu wa wapige kura ya hapana kwa Rais Kikwete

Vipeperushi hivyo, ambavyo vilitawanywa katika maeneo mbalimbali ya mji wa Dodoma vilikuwa na ujumbe unaosomeka: “CCM inayumba,  kwa pamoja tumpunguzie mzigo mheshimiwa Rais kwa kumvua  kofia moja ya uenyekiti, nina imani kwa pamoja tutashinda, piga kura ya hapana kwake, CCM oyeeee.”

Hata hivyo baadhi ya wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM kupitia kundi la vijana, walisema kuwa watamlinda kwa gharama yoyote Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete pamoja na kuhakikisha kuwa anapata kura zote za ‘ndiyo.’

Mbali na hilo, vijana hao walisema kuwa watafanya kila njia kumsaka mtu aliyetengeneza vipeperushi hivyo vinavyosambazwa dhidi ya mwenyekiti wao,  Rais Jakaya Kikwete.
Kikwete akiongoza kikao cha Kamati kuu hapo jana

Wajumbe hao saba kati ya kumi waliitisha mkutano na waandishi wa habari katika Ofisi za CCM Mkoa wa Dodoma na kutoa tamko hilo, huku wakieleza kuwa hawatalala hadi watakapoona mwenyekiti wao akiibuka na ushindi wa kishindo.

“Sisi ndiyo jeshi la chama. Itakuwa ni aibu kama mwenyekiti wetu atakuwa akidhalilishwa kwa kupata kura chache, ilhali nasi tupo. Lazima kuwaaibisha watu wa aina hiyo na kuwasaka popote walipo. Tunaomba vijana wenzetu watuamini kuwa tuko Dodoma kufanya kazi hiyo,” alisema Jery Silaa kwa niaba ya wenzake.

Naye Katibu Mwenezi wa CCM Mkoa wa Kagera,  Hamimu Omary,  amekanusha uvumi uliozagaa kuwa Mkoa wa Kagera ni mmoja ya mikoa inayounga mkono mkakati wa kumhujumu Mwenyekiti wa CCM, Rais Kikwete.

2 comments:

oakleyses said...

chanel handbags, burberry outlet online, christian louboutin outlet, nike air max, oakley vault, tiffany and co jewelry, michael kors outlet online, michael kors handbags, burberry outlet online, ray ban sunglasses, michael kors outlet store, prada handbags, oakley sunglasses, kate spade outlet, christian louboutin shoes, michael kors outlet, longchamp handbags, christian louboutin, coach outlet store online, true religion outlet, louis vuitton outlet, longchamp outlet online, nike free, true religion, polo ralph lauren outlet, gucci handbags, louis vuitton handbags, coach outlet, louis vuitton outlet, prada outlet, nike air max, jordan shoes, nike outlet, polo ralph lauren, louis vuitton, longchamp outlet, red bottom shoes, tory burch outlet online, kate spade outlet online, michael kors outlet online, coach purses, ray ban outlet, michael kors outlet online, coach outlet, tiffany jewelry, cheap oakley sunglasses, louis vuitton outlet online

oakleyses said...

ferragamo shoes, soccer shoes, nike roshe, nfl jerseys, vans outlet, jimmy choo shoes, beats headphones, reebok shoes, valentino shoes, lululemon outlet, birkin bag, p90x workout, ugg outlet, asics shoes, mac cosmetics, longchamp, hollister, mcm handbags, ugg, babyliss, marc jacobs outlet, north face jackets, insanity workout, celine handbags, soccer jerseys, uggs on sale, canada goose outlet, wedding dresses, uggs outlet, replica watches, uggs outlet, canada goose, nike huarache, north face jackets, ugg boots clearance, mont blanc pens, instyler ionic styler, herve leger, nike trainers, canada goose outlet, canada goose outlet, giuseppe zanotti, new balance outlet, bottega veneta, ghd, ugg boots, chi flat iron, abercrombie and fitch, ugg soldes