Monday, November 26, 2012

Pigo jingine!!! Sharobaro Millionea afariki kwa ajali




Habari ambazo zimetufikia hivi punde zinasema Msanii maarufu wa michezo ya kuchekesha ambaye pia  ni mwanamuziki wa Bongo Flava Hussein Mkiety maarufu kwa  Sharo baro Millionea amefariki dunia katika ajali ya gari iliyotokea  huko Muheza mkoani Tanga.

Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Tanga Constantine Masawe ,Hussein amefariki jioni hii katika eneo la Lusanga Muheza.
Msikilize kamanda wa Polisi afafanua kuhusu kifo hicho