Saturday, December 22, 2012

Taifa Stars yaifanyia kweli Zambia yailaza 1 - 0



TIMU ya soka ya Taifa, Taifa Stars jioni hii imewachapa mabingwa wa Afrika, Zambia bao 1-0 katika mechi ya kirafiki ya kimataifa ya soka iliyochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Shujaa wa Taifa Stars katika mechi hiyo alikuwa mshambuliaji Mrisho Ngasa aliyefunga bao hilo la pekee na la ushindi katika kipindi cha kwanza.



Ngasa alifunga bao hilo kwa shuti kali akiwa pembeni ya uwanja, ambalo liligonga mwamba wa juu wa goli na kutinga wavuni.

Katika mechi hiyo, mchezaji aliyeng'ara kwa upande wa Taifa Stars alikuwa kiungo Salum Abubakar 'Sure Boy', ambaye aliumiliki vyema mpira na kucheza atakavyo, hali iliyosababisha wakati mwingine Wazambia waogope kumfuata kwa hofu ya kuaibika.

Mbali na Sure Boy, kiungo mwingine Frank Domayo naye alicheza vyema nafasi ya kiungo mshambuliaji, akishirikiana vyema na Mwinyi Kazimoto na Ngasa, ambao walikuwa mwiba kwa mabeki wa Zambia.

Amri Kiemba alilazimika kucheza mechi hiyo akiwa majeruhi, lakini aliweza kuelewana vyema na wenzake japokuwa hakuwa na kasi iliyozoeleka. Taifa Stars ilikwenda mapumziko ikiwa mbele kwa bao 1-0.

Zambia ilikianza kipindi cha pili kwa kufanya mabadiliko ya wachezaji watano kwa mpigo kabla ya kuongeza wengine wawili kadri dakika zilivyokuwa zikiyoyoma. Walipotaka kuingiza wachezaji wengine wawili, mwamuzi Kirwa kutoka Kenya aliwakatalia.

Katika kipindi hicho cha pili, Taifa Stars ilimpumzisha Khamis Mcha na kumwingiza Simon Msuva kabla ya baadaye kuwatoa Ngasa na beki Kevin Yondan na kuwaingiza Amir Maftah na Nadir Haroub Cannavaro.

Wakizungumza na blogu ya liwazozito wakati wa mchezo huo, baadhi ya mashabiki walimpongeza kocha Kim Poulsen kwa uamuzi wake wa kuwachezesha wachezaji vijana wengi na wasiokuwa na majina.

Mshambuliaji Mbwana Samatta na Thomas Ulimwengu, ambao wamekuwa wakidengua kuja kuichezea Taifa Stars, walijikuta wakiwa kwenye wakati mgumu baada ya kuzomewa na mashabiki.
Juma Kaseja, Erasto Nyoni, Shomari Kapombe, Kevin Yondan, Aggrey Morris, Salum Abubakar, Amri Kiemba, Frank Domayo, Mrisho Ngasa/Amir Maftah, Mwinyi Kazimoto, Khamis Mcha/ Simon Msuva.

2 comments:

oakleyses said...

chanel handbags, burberry outlet online, christian louboutin outlet, nike air max, oakley vault, tiffany and co jewelry, michael kors outlet online, michael kors handbags, burberry outlet online, ray ban sunglasses, michael kors outlet store, prada handbags, oakley sunglasses, kate spade outlet, christian louboutin shoes, michael kors outlet, longchamp handbags, christian louboutin, coach outlet store online, true religion outlet, louis vuitton outlet, longchamp outlet online, nike free, true religion, polo ralph lauren outlet, gucci handbags, louis vuitton handbags, coach outlet, louis vuitton outlet, prada outlet, nike air max, jordan shoes, nike outlet, polo ralph lauren, louis vuitton, longchamp outlet, red bottom shoes, tory burch outlet online, kate spade outlet online, michael kors outlet online, coach purses, ray ban outlet, michael kors outlet online, coach outlet, tiffany jewelry, cheap oakley sunglasses, louis vuitton outlet online

oakleyses said...

ferragamo shoes, soccer shoes, nike roshe, nfl jerseys, vans outlet, jimmy choo shoes, beats headphones, reebok shoes, valentino shoes, lululemon outlet, birkin bag, p90x workout, ugg outlet, asics shoes, mac cosmetics, longchamp, hollister, mcm handbags, ugg, babyliss, marc jacobs outlet, north face jackets, insanity workout, celine handbags, soccer jerseys, uggs on sale, canada goose outlet, wedding dresses, uggs outlet, replica watches, uggs outlet, canada goose, nike huarache, north face jackets, ugg boots clearance, mont blanc pens, instyler ionic styler, herve leger, nike trainers, canada goose outlet, canada goose outlet, giuseppe zanotti, new balance outlet, bottega veneta, ghd, ugg boots, chi flat iron, abercrombie and fitch, ugg soldes