Friday, May 3, 2013

Breaking News!!!!!!!!!!! Serikali yafuta matokeo yote ya form IV mwaka 2012

Waziri Mkuu Mizengo Pinda

Serikali imetangaza kuanzia leo kufuta rasmi matokeo yote ya kidato cha nne mwaka 2012 na mitihani yote itasahihishwa upya kwa kutumia utaratibu ule uliotumika katika matokeo ya mwaka 2011.

Akisoma  bungeni kwa niaba ya Waziri Mkuu ripoti ya awali ya Tume ya kuchunguza kushuka kwa matokeo  ,waziri wa Uratibu na Bunge Williamu Lukuvi amesema hatua hiyo inatokana na uamuzi wa Baraza la Mawaziri ambao waliopokea taarifa ya tume hiyo ambayo imependekeza hatua hiyo.

Kwa mujibu wa Tume hiyo, imependekeza mtihani wa kidato cha nne kusahihishwa upya huku ikiyafuta yale yaliyotangazwa kwa ajili ya kuweka usahihi na njia ya kuelekea kilele cha ubora wa elimu ya Watanzania wote.

Akizungumza Bungeni leo mjini Dodoma, Lukuvi alisema kuwa mitihani hiyo inapaswa kusahihishwa kwa kufuata kanuni ya mwaka 2011, hivyo uamuzi huo umetolewa na Tume ya Waziri Mkuu Pinda aliyounda baada ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi kutangaza matokeo ya kidato cha nne huku asilimia 60 ya wanafunzi wote kufeli.

Suala hilo liliibua mtafaruku mkubwa kwa wadau na wanasiasa wa Tanzania, wakililia haki ya mtoto wa Tanzania kusoma, huku wakisema kufeli kwao kutaongeza joto la maisha magumu kwa watoto hao ambao wengi wanatoka kwenye familia masikini.

Taarifa zaidi ya Tume hiyo na uamuzi wako itaendelea kukujia katika blog yako hii, kwa ajili ya kukufikishia habari kamili na namna ya kuwapatia haki ya kupata elimu watoto wa Tanzania.




No comments: