Friday, August 5, 2011

Hali ni mbaya Somalia , njaa sasa mauaji

Wasomali wauawa katika uvamizi


Mtoto ambaye ni mkimbizi wa ndani akila huko Mogadishu

Takriban watu watano wameuawa na wengine wengi kujeruhiwa baada ya watu wenye silaha kuvamia kambi na kuiba chakula kwenye mji mkuu wa Somalia.

Wakazi wa kambi ya Badbaado, nje ya Mogadishu, walikuwa wamepanga foleni kupata msaada wakati shambulio hilo lilipotokea.

Haikujulikana wazi ni nani alihusika na shambulio hilo japo taarifa nyingine zilisema ni askari wa serikali.
Maelfu ya Wasomali walioathirika na ukame wamewasili kwenye mji mkuu wakisaka chakula.
Katika kipindi cha miezi miwili ya nyuma peke yake takriban wakimbizi 100,000 wamefika kwenye mji mkuu huo .

No comments: