Monday, November 5, 2012

Mtibwa yatafuna Simba 2 - 0, Yanga yatakata kwa Azam 2 - 0


Wachezaji wa Yanga wakishangilia baada ya kupata bao
Mshambuliaji wa Yanga Didier Kavumbagu akijaribu kuwatoka mabeki ya Azam na baadae kufunga bao
 Timu ya Simba imepoteza mchezo wake wa kwanza tangu ligi  Kuu ya Tanzania bara ilipoanza msimu huu baada ya kukubali kipigo cha magoli 2 - 0 kutoka kwa wakata miwa wa Mtibwa timu ya Mtibwa Sugar..

Wakati Simba kipata kipigo hicho wenzao Yanga walitamba Ice cream almaaruf (shikirimu ) za  Azam pale ilipoibanjua kwa jumla ya magoli 2 - 0 katika mechi iliyochezwa kwenye uwanja wa Taifa mjini Dar es Salaam.
Kwa matokeo hayo Yanga sasa imepanda kileleni mwa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara ambapo
 imefikisha pointi 26, na kuizidi Simba ambayo sasa ina pointi  23 na kushika nafasi ya Pili.
Simba itamaliza mzunguko wa kwanza wa ligi kwa kumenyana na Toto African uwanja wa Taifa, Dar es Salaam


1 comment: